Vyakula muhimu kwa mama mjamzito

Lishe bora kwa mama mjamzito ndio nguzo kuu ya ukuaji na maendeleo bora ya mama na mtoto. Miongoni mwa kundi muhimu zaidi la chakula kwa mama mjamzito ni vitamini muhimu. 

Virutubisho hivi ni muhimu sana kwa wajawazito hasa katika miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito.

Umuhimu wa virutubisho hivi vya vitamini kwa mjamzito unatokana na kazi muhimu za virutubisho katika ukuaji wa ujauzito.

Baadhi ya kazi muhimu za virutubisho hivi vya vitamini kwa mama mjamzito ni pamoja na;

  • Kutengenezwa damu hasa kwa mama mjamzito,
  • kuimarisha afya ya ngozi kwa mama na mtoto,
  • ukuaji wa ubongo wa mtoto,
  • ukuaji wa mifupa na misuli ya mtoto,
  • afya ya macho ya mama na mtoto,
  • kuimarisha kinga na ukuaji wa seli za mwili.

Kuna aina kadhaa za virutubisho hivi vya vitamini, ambapo kwa sehemu kubwa ni salama kwa mjamzito ingawa kuna baadhi ya vitamini vinapaswa kudhibitiwa kiwango chake kwa kuwa vinaweza kuleta madhara makubwa kwa mjamzito na mtoto aliyeko tumboni.

Mfano; 

Vitamini A ni muhimu lakini ikiwa vitatumiwa kupita kiwango vinaweza kusababisha matatizo ya kiafya kwa mama na mtoto.

Vyakula muhimu  kwa mama mjamzito.

Sehemu hii ya Makala itaelezea baadhi ya virutubisho muhimu vya vitamini kwa mjamzito, kiwango kiwango kinachostahili, vyanzo muhimu vya aina husika ya vitamini na faida zake kwa mjamzito.

#1: Vitamini A (retinol)

Faida kuu za vitamini A ni kusaidia ukuaji bora wa seli za mwili, macho, ngozi, damu na kuimarisha kinga ya mwili, hivyo kumkinga mjamzito na mtoto dhidi ya maradhi.

Wastani wa kawaida wa matumizi ya vitamini A kwa mjamzito ni kati ya 10000IU/kg hadi 20000IU/kg kwa siku.

Vyanzo vikubwa vya virutubisho hivi vya vitamini A

  • Samaki, 
  • karoti, 
  • brocoli na 
  • nyama.

#2: Vitamini B1 (Thiamine).

Faida za vitamini B1 NI Kusaidia ukuaji wa ubongo wa mtoto, moyo na mfumo wa fahamu.

Wakati wa ujauzito uhitaji wa vitamini hii huongezeka hadi kufikia 1.3mg kwa siku sawa na gramu 250 za nyama ya ngombe au 200gm za vyama ya nguruwe, pia sawa na gramu 300 za njegele.

Vyakula vinginevyo ambavyo ni chanzo kikuu cha vitamini B1 ni 

  • ngano na 
  • amila.

#3: Vitamini B2 (Riboflavin).

Faida za vitamin B2 ni kusaidia maendeleo ya ukuaji ya mtoto tumboni. Mjamzito anapaswa kutumia si chini ya 1.6mg ya vitamini B2 kwa siku.

Chanzo kikuu cha aina hii ya vitamini ni vyakula vya 

  • Maini 
  • soya na 
  • uyoga.

#4: Vitamin B9 (folic acid).

Moja ya vitamini muhimu zaidi kwa mjamzito na mwanamke anayejiandaa kupata ujauzito.

Aina hii ya vitamini ni muhimu kwa sababu husaidia utengenezwaji wa damu ili kukidhi hitaji la ongezeko la damu kwa mjamzito. Vilevile husaidia kuimarisha mfumo wa fahamu na ubongo.

Upungufu wa vitamini hii kwa mjamzito hupelekea mtoto kuzaliwa na matatizo mengi ikiwemo mtindio wa ubongo.

Kwa bahati mbaya miili yetu haina uwezo wa kutengeneza aina hii ya vitamini. Kwa hivyo mjamzito anapaswa kuipata kutoka katika vyakula na virutubisho maalumu.

Kiwango kinachotakiwa kwa mjamzio ama mwanamke anayetarajia ujauzito ni kati ya (300-400) microgramu. Kiwango hiki ni kikubwa kuweza kupatikana kwa namna ya kawaida kupitia vyakula.

Kwa hivyo mjamzito anapaswa kutumia virutubisho vya ziada vya vitamini hii kwa muda wa mwezi mmoja wa kwanza wa ujauzito mfululizo.

Baadhi ya vyakula vyenye virutubisho hivi vya vitamini B9 ni 

  • ndimu, 
  • machungwa na 
  • limao.

#5: Vitamini B6 (pyridoxine).

Vitamini hii husaidia ufanyaji kazi wa mwili katika seli, ukuaji wa ubongo na mfumo wa fahamu. Kiwango cha matumizi kwa mjamzito ni 2.2mg kwa siku.

vyanzo vikuu vya aina hii ya vitamini B6 ni 

  • Njegere, 
  • ndizi, 
  • kuku na 
  • viazi.

#6: Vitamin B12 (cobalamin).

Hii ni vitamini muhimu ambayo husaidia katika kufanikisha utengenezwaji wa damu mwilini. Inapaswa kuwa kwa kiwango kikubwa ili kufanikisha ongezeko la damu kwa mjamzito.

Upungufu wa vitamini hii husababisha tatizo la upungufu wa damu (anemia) kwa mjamzito ikiwa hataongeza matumizi ya vitamini hii.

Mjamzito anapaswa kutumia vyakula vyenye vitamini hii kwa wingi ama kutumia virutubisho maalumu ili kuhakikisha kiwango cha vitamini hii mwilini kinakuwa katika uwiano sahihi.

Chanzo kikuu cha aina hii ya vitamini B12 ni pamoja na 

  • Nyama nyekundu (ng’ombe, nguruwe au mbuzi) 

#7: Vitamin C (ascorbic acid).

Vitamini C ni muhimu kwa sababu husaidia kuimarisha kinga ya mwili kwa mjamzito, husaidia kufyonzwa kwa madini joto ya chuma, kuimarisha tishu za misuli na mifupa laini ya mwili hasa kwa mtoto anaekua.

Kiwango kinachopendekezwa kitaalamu kwa mjamzito ni 80mg kwa siku.

Matunda hasa yenye asili ya uchachu ndio chanzo kikuu cha vitamini C. Baadhi ya matunda hayo ni 

  • beriberi, 
  • machungwa, 
  • limao na 
  • nyanya.

Vilevile baadhi ya mbogamboga kama brocoli na kabeji ni chanzo kizuri cha vitamini C.

#8: Vitamin D (Calciferol).

Hii ni muhimu katika kuimarisha afya ya ngozi ya mjamzito, lakini pia ukuaji wenye afya wa ngozi ya mtoto aliyeko tumboni.

Mwili huzalisha vitamini hii kupitia ngozi, uzalishwaji wa vitamini D mwilini kupitia ngozi unategemea sana mwanga wa jua hasa ule wa jua la saa 12 asubuhi.

Lakini mbali na mwili kuwa na uwezo wa kutengeneza vitamini D, mahitaji ya mjamzito huwa ni makubwa kiasi kwamba utengenezwaji wa itamini D katika ngozi pekee haukidhi mahitaji.

Mjamzito anashauriwa kutumia vyakula vyenye kiwango kikubwa cha vitamini D kadri awezavyo.

Mafuta ya samaki ndio chakula pekee asili ambacho tunaweza kupata vitamini D. Kwa mjamzito anashauriwa kutumia virutubisho maalumu vya vitamini D ikiwa itahitajika.

#9: Choline.

Kirutubisho hiki si vitamini wala madini joto lakini ni muhimu sana kwa mjamzito na mtoto aliyeko tumboni.

Kirutubisho hiki husaidia katika utengenezwaji na ukuaji wa seli a mjamzito na mtoto, ukuaji wa ubongo, ugwemgongo na mfumo wa fahamu kwa ujumla.

Pia husaidia utengenezwaji na ufanyaji kazi wa viamshi vya umeme mwilini ambavyo hufanya kazi ya kusafilisha taarifa mbalimbali katika mwili.

Virutubisho hivi hupatikana zaidi katika vyakula vifuatavyo

  • Spinachi,
  • Maziwa,
  • Soya,
  • Samaki,
  • Ndizi na
  • Ngano.

Muhimu kuhusu vyakula vya mjamzito.

Hivi ni vyakula muhimu kundi la vitamini ambalo mjamzito anapaswa kutumia katika kiwango elekezi ili kuimarisha afya yake lakini pia kuimarisha afya na ukuaji bora wa mtoto aliye tumboni.

Mambo mengi yanaweza kuathiri upatikanaji na ufuatiliaji wa mlo kamili kipindi cha ujauzito huku kubwa likiwa ni uchumu wa familia.

Katika kutambua hilo afya plus tumekukuchambulia na kukupendekezea vyakula na nyanzo mbalimbali vya virutubisho hivi ambavyo ni rahisi na nafuu zaidi kupatikana.

Kumbuka mtoto ni zawadi kubwa katika maisha na ndio huleta dhana nzima ya maisha na furaha katika familia. Hakikisha unapata watoto wenye afya na timamu kwa kuzingatia ushauri na mapendekezo ya kitaalamu.

Hakikisha unahudhuria kliniki kwa ajili ya uratibu wa ujauzito wako lakini pia mshirikishe mtaalamu wa afya anayeratibu ujauzito wako ikiwa kuna jambo au ushauri wowote wa kitaalamu.

 

Next Post Previous Post
No Comment
Andika Swali au Maoni
comment url