Dawa za asili za kutibu fangasi za ukeni
Baada ya kutazama dawa za kisasa za kutibu fangasi za ukeni, katika makala hii tutaangazia dawa za asili/kienyeji za kutibu tatizo la fangasi za ukeni.
Kuna mitishamba, vyakula, madini joto na njia kadhaa za
asili ambazo unaweza kuzitumia kutibu tatizo la fangasi sugu ukeni.
Kama ilivyo kwa njia za kisasa za kutibu fangasi, njia za
asili pia zinaweza kutumika kwa namna 3, yaani kupaka, kupachika na
kumeza/kunywa.
Dawa hizi za asili hufanya kazi katika misingi mikuu
ifuatayo:
- Kutibu matatizo au sababu zilizopelekea fangasi za ukeni kutokea
- Kudhibitiukuaji wa moja kwa moja wa fangasi wa Candida albicans
- Kusaidia kuweka hali ya uke katika msawazo wa chaji
- Kusaidia au kupunguza miwasho, michubuko na uvimbe katika uke
- Kuimarisha kinga ya mwili
- Kudhibiti uzalishwaji wa ute ukeni
Dawa za asili za fangasi za ukeni
Faida kubwa ya kutumia njia za asili za kutibu fangasi ukeni
ni uwezekano mdogo wa fangasi hawa kutengenezwa usugu wa dawa hizi.
Ili kuongeza ufanisi wa dawa hizi unashauriwa kutumia zaidi
ya njia moja ya asili katika kupambana na tatizo la fangasi sugu.
Zifuatazo ni dawa asili za kutibu fangasi sugu za ukeni:
01: Matumizi ya Boric acid
Boric acid ni kemikali ya asili ambayo hupatikana katika
mazingira yetu. Kemikali hii imeundwa na elementi za Boron, Hydrojeni na
Oksijeni.
Kemikali hii ina nguvu na uwezo wa kuangamiza vimelea wa
aina mbalimbali ikiwemo fangasi, bakteria na virusi.
Jinsi ya kutumia boric acid kutibu fangasi za ukeni
Kemikali huu hutumiwa kwa kupachika ukeni, inapatikana katika muundo wa vidonge na unga.
Tumia kidonge cha boric acid kwa kupachika
ukeni na kukiacha kwa muda usiopungua masaa 8 hasa nyakati za usiku.
Kemikali hii hupatikana katika maduka ya dawa ya dawa katika muundo wa vidonge au unga.
Unaweza kununua unga na kutengenezwa kidonge, lakini
hakikisha unapata maelekezo muhimu juu ya namna gani unaweza kutengenezwa
kidonge kutokana na unga wa boric acid.
Boric acid inasaidia kuondoa muwasho, michubuko na kuwaka mlinganyo mzuri wa hali ya uke.
02: Kitunguu saumu
Kitunguu saumu ni miongoni mwa mimea ambayo ina uwezo wa
kipekee wa kuangamiza vimelea mbalimbali wa magonjwa kwa ufanisi mkubwa.
Tafiti mbalimbali zimethibitishwa uwezo wa Kitunguu saumu
katika kutibu fangasi hususa ni fangasi sugu.
Jinsi ya kutumia Kitunguu saumu kutibu fangasi sugu za ukeni
Kitunguu saumu hutumika kutibu fangasi za ukeni kwa
kupachika punje zake ukeni.
Unachotakiwa kufanya ni kumenya punje ya Kitunguu kisha
ipachike ukeni, hakikisha unaisukumia ndani kadri uwezavyo.
Acha kwa muda usiopungua masaa 8 kabla ya kutoa, wakati wa
usiku ni bora zaidi.
Ili kurahisisha matumizi ya Kitunguu saumu unaweza kupaka
mafuta ya mimea kama vile nazi au alizeti, katika punje ya Kitunguu ili
kurahisisha uingiaji wake katika uke.
Kitunguu saumu ni tiba bora hasa kwa fangasi sugu za ukeni
na inafanya kazi kwa kuua vimelea hawa wa fangasi.
03: Mimea ya Goldenseal, Goldthread, na Oregon Grape Root
Mimea hii yote ina kemikali za berberine na palmatine,
kemikali hizi zina uwezo wa kuangamiza fangasi na vimelea mbalimbali wa
magonjwa.
Goldenseal unatajwa kuwa na ufanisi zaidi na unaweza
kutumiwa peke yake.
Jinsi ya kutumia Goldenseal
Unaweza kuandaa mzizi wa mmea huu na kuuloweka kwenye maji
ya moto kwa muda wa dakika 10 hadi 20.
Kisha tumia maji yenye mchanganyiko huu kwa kuoshea uke mara
1 kwa siku 3 hadi 5.
Mmea huu pia unapatikana katika muundo wa vidonge au unga.
Tumia kidonge kwa kupachika ukeni.
Vilevile unaweza kununua unga wa Goldenseal kisha ukatengeneza kidonge chake mwenyewe.
Hakikisha unapata ushauri na maelekezo
muhimu ya kutengenezwa kidonge hiki kutoka kwa mfamasia.
Mbali na kutumia katika muundo wa vidonge, mimea hii pia
inaweza kutumiwa kwa kunywa.
Muhimu
Mimea hii haipaswi kutumiwa na wajawazito kwa sababu inaweza kusababisha mimba kuharibika.
Jambo lingine la muhimu kufahamu ni kwamba utumiapo mimea hii kwa nia ya kupachika, inasababisha uke kutoa ute wa manjano.
Ute huu ni salama na unatokana na kemikali za berberine ndani ya mimea hii.
04: Mafuta ya mti wa chai (Tea tree)
Mafuta kutoka katika mmea huu ni moja ya dawa muhimu za
kutibu fangasi ukeni.
Matumizi ya vidonge vya kupachika vinavyotengenezwa na
mafuta haya kwa siku 5 yameonyesha uwezo mkubwa wa kuangamiza jamii mbalimbali
ya fangasi zinazoathiri uke.
Unaweza kupata mafuta haya katika maduka mengi ya dawa za
kisasa au dawa za asili.
05: Matumizi ya maziwa mgando (Yoghurt) yenye bakteria wa Lactobacillus
Bakteria wa Lactobacillus husaidia kuleta mlinganyo wa
vimelea wa faida mwilini wakiwemo vimelea wa candida albicans ambao hupatikana
kwa wingi katika uke.
Matumizi ya vyakula vyenye bakteria hawa husaidia kuongeza
bakteria hawa mwilini na kusaidia kuleta mlinganyo wa vimelea wa fangasi katika
uke.
Wanawake wenye tatizo la fangasi ukeni wanashauriwa kutumia yoghurt
kwa kiasi kikubwa.
06: Matumizi ya mmea wa Orbukoi (Terminalia mollis)
Orbukoi ni jina la kimasai, mmea huu unapatikana maeneo mengi
ya Tanzania na ni miongoni mwa tiba bora za fangasi aina zote.
Tumia mmea huu kwa kutengenezwa kuloweka mizizi, magome na
majani laini katika maji ya moto kwa dakika zisizopungua 15.
Chuja na subiri mchanganyiko uwe wa vuguvugu kisha tumia kwa
kuosha uke wako, mara moja kwa siku kwa muda siku 5 hadi 14.
Mbali na kutibu fangasi mmea huu ni miongoni mwa mimea
michache yenye uwezo wa kuangamiza virusu vya UKIMWI.
07: Matumizi ya mmea wa Mkulo (Ocotea usambarensis)
Mmea huu pia hujulikana kwa jina la Mseri (kichaga) na muheti
(kihehe). Mafuta ya mmea huu yanaweza kutumika kutibu fangasi za ukeni katika
muundo wa vidonge vya kupachika.
Vilevile unaweza kuchanganya mafuta haya na mafuta ya
alizeti, mzeituni au nazi na kutumia kwa kupaka ukeni.
Mimea mingine ya kutibu fangasi ukeni ni pamoja na:
- Mkunazi (Bafalo thorn), hujulikana pia kama Olelailai kwa kimaasai: Juisi ya magome, mizizi na majani hutumika kuoshea uke.
- Licorice: Vidonge vinavyotokana na unga wa mizizi ya mmea huu hupachikwa ukeni au juisi ya mizizi ya mmea huu unaweza kutumia kuoshea uke.
- Calendula, mizizi ya mmea wa Comfrey, Lavender, mizizi ya mmea wa Marshmallow: mimea hii ndio inatajwa kuwa na Ufanisi wa hali ya juu katika kutibu magonjwa ya ngozi ikiwemo Fangasi.
Wasiliana na Mfanasia au mtaalamu wa mitishamba ili kupata
ushauri sahihi wa namna na kiwango sahihi cha kutumia mimea hii.
Hitimisho
Hizi ni baadhi ya njia za asili za kutibu fangasi za ukeni, kwa
sehemu kubwa njia hutumika kwa njia ya kupachika ukeni, ingawa baadhi zinaweza
kutumika kwa njia ya kuoshea uke.
Hata hivyo, kutibu fangasi za ukeni kwa kutumia dawa hizi kwa
njia ya kuosha uke si salama kutokana na sababu kwamba dawa hizi zinaua kiasi
kikubwa cha vimelea wa faida mwilini, lakini pia maangalizi ya dawa hizi yanaweza
yasiwe salama kiasi cha kupeklekea maambukizi zaidi.
Iwapo unafikiria kutumia njia hizi za asili ili kutibu fangasi za ukeni hakikisha unapata ushauri sahihi kutoka kwa mfamasia au daktari.